Kwa mujibu wa Kitengo cha tarjama cha Shirika la Habari la Hawza, kundi la mashabiki lilituma barua yenye anuani isemayo “Simamisheni Mchezo” kwa shirikisho hilo, ambayo ilisainiwa na wachezaji wa Ligi ya Ireland. Miongoni mwa waliotia saini ni Brian Kerr, kocha wa zamani wa timu ya taifa, na Louise Quinn, mchezaji wa zamani na mshindi mara mbili wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa wanawake.
Roberto Lopez, Rais wa Chama cha Wachezaji wa Kulipwa wa Soka Ireland alisema: “Hatuwezi kupuuza janga la kibinadamu nchini Palestina; kupotea kwa maisha ya watu huko Ghaza kunapaswa kutangulia mbele ya aina yoyote ya masuala ya kimichezo.” Pia walitangaza kwamba Ireland, iwapo itakubali kufanyika kwa mechi katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina, itakuwa imekiuka sheria za UEFA na FIFA.
Chanzo: Dearborn
Maoni yako